FAHAMU JINSI YA KUOMBA SALA YA VITA


 

SALA YA VITA (0766500747)

Namuungamia Mungu Mwenyezi kutokana na dhambi zangu zote nilizokutenda Bwana kwa mawazo yangu, kwa vitendo vyangu na kutotimiza wajibu wangu, Bwana unisamehe, naomba msamaha wa dhambi zangu kwa jina takatifu la Yesu Kristo Mwokozi wangu, natangaza uhuru wangu kwa damu ya Yesu Kristo wa Nazareth.

Nakuja kwa Baba Mtakatifu, Mungu wangu katika jina takatifu litetemeshalo mpaka kuzimu la Bwana wetu Yesu Kristu, naomba unijalie moyo wa ujasiri, nguvu na imani katika sala hii, nipe ujasiri kama mtumishi wako Daudi katika vita na Goliati, univalishe nguvu na imani kutoka mbinguni kwa msingi wa neno lako.

Sasa Mwenyezi Mungu natumia moyo wa ujasiri, nguvu na Imani uliyonijalia kupiga na kuteketeza milele mipango yote ya shetani na mawakala wake dhidi yangu, na dhidi yah ii kazi yangu na familia yangu yote katika jina la Yesu Kristo.

Baba nipe mpako wa kivita kama uliompa Daudi zaburi 89:20-24 inashuhudia na ahadi yako yasema “mimi nitawaponda wapinzani wake, nitawaangamiza wote wanaonichukia” kwa neno hili Mwenyezi Mungu nawakabidhi maadui zangu wote mbele yako.

Baba Mungu Mwenyezi navaa silaha za vita kama ilivyoandikwa (waefeso 6:10-18) navaa ukweli kama mkanda kiunoni mwangu, navaa uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani, hamu ya kutangaza habari njema na amani iwe kama viatu miguuni pangu, imani iwe ngao mikononi mwangu kama kofia ya chuma na neno la Mungu kama upanga niliopewa na roho Mtakatifu dhidi ya maadui zangu.

Nathibitisha neno la Mungu ni kweli na nachagua leo kuishi katika mwanga wa neno hilo, fungua macho yangu Bwana unionyeshe maeneo ya maisha yangu yasiyokupendeza na maadui wangu wote waangaziwe nuru yako, na ninabomoa leo katika maisha yangu makao yote ya shetani na kuangamiza mipango yote ya shetani ambayo ameipanga ndani yangu, ameijenga ndani yangu dhidi ya akili yangu, afya yangu, taaluma yangu, kazi yangu, mme wangu, utashi wangu, maeneo yangu, hisia zangu na mwili wangu.

Navaa mamlaka Bwana kwa neno lako toka Mathayo 18:18 ninatuma neno hili kufunga nguvu zote za shetani na mawakala zake wanaojidhihirisha katika maisha yangu kwa jina la Yesu Kristo, nawafunga na kuwagombanisha wao kwa wao mpaka watakapokiri kwa vinywa vyao na matendo yao kuwa Yesu Kristo ni Bwana.

Nateketeza nguvu zote za giza katika kazi yangu na nyumbani ninamoishi na eneo lote bila kujali zimejificha wapi iwe hewani, angani, motoni, ardhini, baharini, chini ya bahari, chini ya ardhi naziteketeza zote kwa jina la Yesu, nakuja kinyume na pepo wakuu wote wa uovu katika nchi hii, mji huu, nyumba hii na katika eneo langu la kazi kwa jina la Yesu Kristo.

Nafunga mapepo yote na nguvu yote ya kishirikina na uchawi inayotumika na watu hawa walioumbwa kwa sura ya mfano wa Mungu, nafunga nguvu zako zote wewe (Taja maadui kwa majina yao) na kundi lenu lote, nawaweka wote chini ya msalaba wa Kristo katika jina la Yesu mpaka pale mtakapokili Yesu Kristo ni Bwana.

Kwa nguvu za Mwenyezi Mungu nawatangazia msamaha kwa yale yote mlionitendea, maana nguvu zako Mungu wangu na ulinzi wako umejidhirisha juu ya maisha yangu na kwa jina la Yesu nakuja kinyume na kusanyiko lolote la kichawi katika eneo langu la kazi, shule yangu, nyumba yangu kuanzia angani, motoni, ardhini, chini ya ardhi, baharini, chini ya bahari, karibu na nyumba hii popote pale kwa jina la Yesu Kristo.

Katika jina tukufu la Yesu Kristo, nafunika mahali hapa na eneo hili kwa damu azizi ya Bwana wetu Yesu Kristo, nafunika shule yangu kwa damu ya Yesu Kristo na damu ya Yesu ikawateketeze roho za giza zote katika eneo hili, nafungulia moto war oho mtakatifu ufunike eneo langu lote la kazi, nafungulia ulinzi wa Mungu katika pembe zote za mahali hapa, naangamiza roho zote za visasi kwa jina la Yesu Kristo.

Baba mtakatifu nakupa sifa zote, heshima na utukufu, wafungulia malaika wako wenye nguvu za kivita kushuka na kuweka ulinzi mahali hapa dhidi ya shetani na majeshi yake ya nguvu za giza. Namwaga damu ya Yesu katika maeneo yote ya nyumba hii na wapanga malaika wa Mungu kuyalinda maeneo yote ninamoishi kwa jina la Yesu Kristo.

Baba yetu x 3 salamu Maria x 3 atukuzwe x 3

Mtakatifu Mikael Malaika Mkuu – utuombee

Mtakatifu Raphael Malaika Mkuu – Utuombee

Watakatifu Malaika Wakuu – utuombee

Amina.

UNAWEZA PIA KUTAZAMA VIDEO HIZI ZA SAUTI KWAJILI YA MAFUNDISHO ZAIDI






Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

SALA KWA AJILI YA KUFUNGULIWA KUTOKA KATIKA NGUVU ZA GIZA

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO

IBADA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA