JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA




JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA

 

KANUNI ZA IMANI

1.  Nasadiki kwa Mungu Baba Mwenyezi muumba mbingu na dunia na kwa Yesu Kristo mwanaye wa pekee, Bwana wetu, aliyetungwa kwa uwezo wa roho mtakatifu akazaliwa na Bikra Maria akateswa kwa mamlaka ya Polystyo Pilato, akasulubiwa akafa, akazikwa akashukia kuzimu siku ya tatu akafufuka katika wafu akapaa mbinguni, amekaa kuume kwa Mungu baba Mwenyezi toka huko atakuja kwa utukufu kuwahukumu wazima na wafu, Nasadiki kwa roho Mtakatifu, Kanisa takatifu Katoliki, ushirika wa watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili na uzima wa milele ijayo Amina.

 

2.   BABA YETU

Baba Yetu uliyembinguni jina lako litukuzwe, ufalme wako ufike utakalo lifanyike duniani kama mbingui utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyo wasamehe na sisi waliotukosea usitutiye katika kishawishi lakini utuokoe maovuni Amina.

 

3.   SALAMU MARIA

Salamu Maria umejaa neema Bwana yu nawe umebarikiwa kuliko wanawake wote na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa, Maria mtakatifu mama wa Mungu utuombee sisi wakosefu sasa na saa ya kufa kwetu Amina.

 

4.   ATUKUZWE

Atukuzwe Baba, Mwana na Roho Mtakatifu – Amina.



MAFUMBO YA ROSARI YAKO MANNE NA YANASALIWA SIKU TOFAUTI TOFAUTU, JAPO WAWEZA KUSALI YOTE SIKU MOJA KADRI UWEZAVYO

Pamoja na Rosari kuwa na matendo 4, ambayo kila tendo yemebeba mafumbo 5, hivyo kabla ya kusali au kutamka fumbo (tendo) sala zifuatazo zinatangulia kabla ya fumbo. Ukiwa umeshika punje yako ya fumbo utasali,

-      Atukuzwe Baba x 1

-      Tuwasifu milele Yesu, Maria na Yoseph x 1

-      Ee Yesu mwema utusamehe dhambi zetu utukinge na moto wa milele ongoza roho zote mbinguni hasa za wale wanaohitaji Zaidi huruma yako.

-      Damu ya Kristo iziokoe roho zote toharani izijaliye nuru ya uzima wa milele – Amina

-      Tendo | fumbo (Hapa unataja tendo \ fumbo )

-      Baada ya Tendo utasali Baba yetu kabla ya kuanza tembe kumi za salamu Maria.

MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)

Tendo la kwanza: Malaika Gabriel anapasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu * Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.

Tendo la pili: Bikra Maria anakwenda kumtembelea Elizabeth Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.

Tendo la Tatu: Yesu anazaliwa Bethlehemu* Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara.

Tendo la Nne: Yesu anatolewa hekaluni* Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.

Tendo la Tano: Maria anamkuta Yesu hekaluni*

Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.

 

MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)

Tendo la kwanza: Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu.

Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.

Tendo la Pili: Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu.

Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.

Tendo la Tatu: Yesu anatiwa miiba kichwa kwa ajili yetu.

Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.

Tendo la Nne: Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu.

Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.

Tendo la Tano: Yesu anakufa Msalabani.

Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.

 

MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)

Tendo la kwanza: Yesu anafufuka.

Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.

Tendo la Pili: Yesu anapaa mbinguni.

Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.

Tendo la Tatu: Roho Mtakatifu anawashukia Mitume.

Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.

Tendo la Nne: Bikira Maria anapalizwa mbinguni.

Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.

Tendo la Tano: Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni.

Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.

 

MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)

Tendo la kwanza: Yesu anabatizwa mto Yordani.

Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.

Tendo la Pili: Yesu anageuza maji kuwa divai huko kana.

Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya Injili.

Tendo la tatu: Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu.

Tumwombe Mungu atujalie kupokea ufalme wake wa toba ya kweli.

Tendo la Nne: Yesu anageuka sura.

Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung`arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.

Tendo la Tano: Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristi.

Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.

 

Kila baada ya kumaliza kusali rosary Sali sala hii: SALAMU MALKIA

Salamu, Malkia, Mama mwenye huruma, uzima, tulizo na matumaini yetu, salamu. Tunakusihi ugenini hapa sisi wana wa Eva. Tunakulilia tukilalamika na kuhuzunika bondeni huku kwenye machozi. Haya basi, mwombezi wetu, utuangalie kwa macho yako yenye huruma. Na mwisho wa ugeni huu, utuonyeshe Yesu, mzao mbarikiwa wa tumbo lako. Ee mpole, ee mwema, ee mpendevu, Bikira Maria.

 

·         Kumbuka fumbo linatamkwa na mtu mmoja, mwongozaji na baada ya fumbo maombi au ombi katika fumbo linaitikiwa na watu wote, kama unasali peke yako utataja na ombi wewe mwenyewe kwa kila fumbo.

LITANIA YA BIKIRA MARIA

Bwana, utuhurumie      Bwana, utuhurumie

Kristo, utuhurumie       Kristo, utuhurumie

Bwana, utuhurumie      Bwana, utuhurumie

Kristo, utuhurumie       Kristo, utuhurumie

 

Baba wa Mbinguni, Mungu                    utuhurumie

Mwana, mkombozi wa dunia, mungu     utuhurumie

Roho mtakatifu, mungu                       utuhurumie

Utatu mtakatifu, mungu mmoja            utuhurumie

Maria mtakatifu                                  utuombee

Mzazi Mtakatifu wa Mungu                  utuombee

Bikira Mtakatifu mkuu wa mabikira      utuombee

Mama wa Kristo                                utuombee

Mama wa neema ya Mungu               utuombee

Mama mtakatifu sana                       utuombee

Mama mwenye moyo safi                 utuombee

Mama mwenye ubikira                     utuombee

Mama usiye na dhambi                   utuombee

Mama mpendelevu                        utuombee

Mama msitaajabivu                       utuombee

Mama wa shauri jema                  utuombee

Mama wa Muumba                      utuombee

Mama wa kombozi                      utuombee

Bikira mwenye utaratibu             utuombee

Bikira mwenye heshima             utuombee

Bikira mwenye sifa                    utuombee

Bikira mwenye uwezo                  utuombee

Bikira mwenye huruma                utuombee

Bikira mwaminifu                        utuombee

Kioo cha haki                             utuombee

Kikao cha hekima                       utuombee

Sababu ya furaha yetu                utuombee

Chombo cha neema                   utuombee

Chombo cha heshima                 utuombee

Chombo bora cha ibada             utuombee

Waridi lenye fumbo                   utuombee

Mnara wa Daudi                       utuombee

Mnara wa pembe                     utuombee

Nyumba ya dhahabu                utuombee

Sanduku la agano                   utuombee

Mlango wa mbinguni               utuombee

Nyota ya asubuhi                   utuombee

Afya ya wagonjwa                 utuombee

Kimbilio la wakosefu              utuombee

Mfariji wa wenye uchungu         utuombee

Msaada wa wakristo                 utuombee

Malkia wa Malaika                   utuombee

Malkia wa Mababu                  utuombee

Malkia wa Manabii                  utuombee

Malikia wa Mitume                 utuombee

Malkia wa Mashahidi              utuombee

Malkia wa waungama            utuombee

Malkia wa Mabikira               utuombee

Malkia wa watakatifu wote                                 utuombee

Malkia uliyeumbwa pasipo dhambi ya asili           utuombee

Malkia uliyepalizwa mbinguni                            utuombee

Malkia wa Rozari Takatifu                                utuombee

Malkia wa Amani                                            utuombee

 

Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia                Utusamehe Bwana

Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia                Utusikilize Bwana

Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia             Utuhurumie

 

Tuombe

Ee Bwana tunakuomba utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote, na kwa maombezi matakatifu ya Maria Mtakatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya sasa, tupate nasi furaha za uzima wa milele. Tunaomba hayo kwa ajili ya Kristo Bwana wetu. Amina.


KWA MAFUNDISHO ZAIDI UNAWEZA KUTAZAMA VIDEO HII



 

N:B

Lengo na madhumuni ni kukufanya wewe mkatoliki kujifunza kusali rosary bila shida yoyote.

 

Imeandaliwa na Mwl. Julius Theophil Mmbaga

Simu: 0766 500 747 Mwanza.




          BOFYA HAPA KUTAZAMA VIDEO HII 


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAHAMU JINSI YA KUOMBA SALA YA VITA

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

SALA KWA AJILI YA KUFUNGULIWA KUTOKA KATIKA NGUVU ZA GIZA

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO

IBADA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU