UPAGANI ULIOJIFICHA KATIKA MWAMVULI WA DINI


 UPAGANI ULIOJIFICHA KATIKA MWAMVULI WA DINI

Ndugu zangu wapendwa katika Kristo. Naomba leo kwa pamoja tutafakari huu upagani uliojificha katika mwavuli wa dini.

Upagani kwanza ni nini? Mimi naweza kusema upagani ni ile hali ya kuishi bila kujua uwepo wa Mungu, ni hali ya kuishi katika imani isiyofungamana na Mungu mwenyezi, ni hali ya kutegemea miungu wengine, kutomjua Mungu kabisa.

Ndugu zangu baada ya kujaribu kuelezea upagani kwa tafsiri yangu, hebu tujiulize tena dini ni nini? Dini ni mkusanyiko wa watu wenye imani moja wanaokusanyika pamoja kwa lengo la kumwabudu Mungu wao, kusali na kuomba pamoja, kuna dini za aina nyingi lakini zote zinakusanyika pamoja kwa imani yao kuongea na Baba yetu aliye mbinguni, na dini uanzia ndani ya familia.

Watu wenye dini ujitenga kabisa na mambo ya kipagani utembea na Mungu Muumba nchi na vitu vyote vinavyoonekana na wakiamini Mungu wao anaweza kila kitu, Mungu wao anajitosheleza wala haitaji msaada wowote, hivyo watu wenye dini yaani wenye kuamini uwepo wa Mungu mmoja, daima wakipata changamoto, shida yeyote upiga magoti na kuomba msaada kwa Mungu wao, na Mungu wao ambaye ni Baba yetu aliye mbinguni uwajibu maombi yao, kupitia kwa mwanaye mpendwa Bwana wetu Yesu Kristo.

Watu wenye dini hawafanyi kafara, maana kafara yao ya mwisho ni mwili, damu, roho ya Bwana yetu Yesu Kristo aliyejitoa msalabani kwa ajili ya ukombozi wao. Watu wenye dini uamini kila kitu kinachofanyika ni mapenzi ya Mungu na daima umpa Mungu utukufu, hata kama wanapitia mateso, maangaiko daima uwomba, umtegemea Mungu wao wala hawaabudu katika madhabau yeyote zaidi ya ile ya Mungu wao aliye hai.

Laikini katika watu hawa wenye dini ndani yao kuna mchanganyiko wa wapagani, yaani watu wanaoigiza kwamba Mungu yupo, lakini hawamwamini huyo Mungu kama anaweza kutatua matatizo yao, hawa ni watu wanaopenda kupitia njia fupi ili kupata ufumbuzi wa matatizo yao, hawa ni watu washirikina, wachawi, ni watu wenye kuhudumu katika madhabau ya shetani, ni watu wenye kumtii sana shetani kuliko Mungu, ni watu wenye kiburi cha kuzimu ambacho wanakificha katika mwamvuli wa dini, watu hawa ukiwaona Makanisani ni wanyenyekevu, wengine ni viongozi, ni wa kwanza kanisani, lakini ukichunguza matendo yao, yanaweza kukufanya nawe kufa moyo hata kwenda kusali. Lakini tukumbuke watu wote ni wa Mungu, wawe wapagani, wawe wanadini wote hawa Mungu uwapenda na kuwatendea mema kadri ya mapenzi yake, yaani daima Mungu utimiza mapenzi yake kwetu, changamoto ni kwetu kutimiza mapenzi ya Mungu.

Hivyo tunashuhudia watu hawa ambao leo nawaita ni wapagani maana licha ya kujiita kuwa wanadini, lakini hawatendi yale yawapasayo kutenda wawapo mafichoni/gizani, wanatenda sawa sawa na giza wanafukuza nuru kabisa, watu hawa wamevaa upagani ambao wanauficha ndani ya dini. Maana wanafanya mabo ya kipagani ambayo hayanatofauti na yule asiye mjua Mungu, wanafanya kinyume na amri za Mungu. Hebu tuangaliye watu hawa baadhi ya mambo ya kipagani wanayofanya ili ujue au yawezekana nawe ukawa ni mmoja wapo ili ujifunze na uyaache kabisa na kutembea na Mungu tu, ndani ya dini yako, hapa tunajumuisha mambo yote ya kishirikina – maana yote hayo ni upagani tupu.

1.    Kuacha kumtegemea Mungu na kuabudu mapepo, majini n.k huku kila siku ya kuabudu unakwenda kanisani huo ni upagani.

2.    Kufanya kafara au kutambika kwa kutoa sadaka kwa mashetani ili yakulinde, yakusaidiye, yakupe utajiri n.k huo ni upagani.

3.    Kuzindika nyumba au mji kwa kuweka ulinzi wa kipepo ukiamini Mungu hawezi kabisa. Huu ni nao ni upagani.

4.    Kukata kata mwili wako na kuutoa damu kwa kutumia wembe au kisu kisa kujipakaa dawa nyeusi au rangi yeyote eti ni ulinzi na unakwenda kanisani kusali, huo ni upagani ndani ya dini.

5.    Kuzaa mtoto na kumfanyia matambiko mbalimbali mpaka juu ya jina lake huo ni upagani, badala ya mtoto kumpeleka kanisani na kubarikiwa, kumkabidhi mikononi mwa Bwana, wewe unaanza kumkabidhi mtoto wako kwa shetani huo sio Ukristo ndugu yangu ni upagani.

Mambo yote wewe unayejiita wa Kristo, unakwenda kanisani na Biblia yako, na unafanya mambo yanayofanana na hayo, wewe ni mpagani uliojificha katika mwamvuli wa dini, ukiwa kanisani ni wakwanza kuimba mapambio, huku ukisema Mimi ni Mkatoliki, Mimi ni Mlokole, Mimi ni Msabato, Mimi ni Mlutheri, Ndugu yangu shetani haogopi dini yako, shetani anaogopa imani yako thabithi katika dini yako, na wala wewe kuwa Mlokole au dini yoyote sio kibali cha wewe kwenda mbinguni, Mungu anaona matendo yako, Imani yako, hivyo kutuigizia sisi wanadamu ambao hatuji matendo yako unayoyafanya ufichoni, matendo ya kipagani, Mungu anakuona, kuvaa mwamvuli wa dini mbele yetu ni maficho ya muda mfupi sana maana Mungu anakuona, siku ile ikifika utasema, Mimi nilikuwa Mchungaji, nilikuwa Sister, Nilikuwa Padri, nilikuwa Mwamini mzuri kabisa na nilikutumikia, ndipo hapo matendo yako yote yataonekana wazi maana Mungu wetu ni Mungu wa haki kamwe haoneii mtu na huruma yake haina mipaka, atakuonyesha matendo yako yote na utapokea hukumu yako sawa sawa na haki yako.

Hivyo niitimishe kwa kusema wewe ambaye unamdanganya Mungu, jua unajidanganya mwenyewe, usitudanganye sisi ambaye hatukujui vema, tunakushangilia na kukupa cheo ndani ya kanisa kumbe wewe ni Mchawi, yote unayofanya katika Mwamvuli wa dini yako yana mwisho wake.

Mungu atubariki sana.

Imeandaliwa na:

Mtumishi, Julius Mmbaga

0766500747

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAHAMU JINSI YA KUOMBA SALA YA VITA

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

SALA KWA AJILI YA KUFUNGULIWA KUTOKA KATIKA NGUVU ZA GIZA

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO

IBADA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA