TUSALI SALA YA ASUBUHI


 

TUSALI SALA YA ASUBUHI

 

+Kwajina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

 

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu mmoja, sasa na siku zote na milele amina. Ee utatu Mtakatifu wa Mwenyezi Mungu; +Baba, +Mwana na +Roho Mtakatifu. Ninasadiki kuwa upo hapa na mahali pote.

 

Ee Mungu wangu, umeniumba, umenikomboa, umenifanya mkristu, umenizidishia neema zako, umenitayarishia makao yangu mbinguni.

Ee Mungu wangu, nakuabudu, nakushukuru, nakuomba toba, nakupenda. Ee Mungu wangu, ninakutolea roho yangu, na mawazo, na maneno, na kazi na furaha, na mateso yangu, uyapokee unipe neema yako nisitende leo dhambi, Amina.

______________________

Ee Baba yetu Mungu mkuu,

Umenilinda usiku huu.

Nakushukuru kwa moyo,

Ee Baba, Mwana na Roho.

Nilinde tena siku hii,

Niache dhambi, nikutii.

Naomba sana Baba wee,

Baraka zako nipokee.

Bikira safi, Ee Maria

Nisipotee nisimamie.

Mlinzi mkuu malaika wee,

Kwa Mungu wetu niombee

Nitake nitende mema tu,

Na mwisho nije kwako juu. Amina.

 

NIA NJEMA.

Kumheshimu Mungu wangu

Namtolea roho yangu,

Nifanye kazi nipumzike

Amri zake tu nishike

Wazo, neno, tendo lote

Namtolea Mungu pote

Roho, mwili chote changu,

Pendo na uzima wangu

Mungu wangu nitampenda,

Wala dhambi sitatenda.

Jina lako nasifia,

Utakalo hutimia.

Kwa utii navumilia

Teso na matata pia.

Nipe, Bwana, neema zako

Niongeze sifa yako. Amina.

 

•SALA YA MATOLEO.

Ee Yesu, kwa mikono ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sala, matendo, masumbuko na furaha zangu zote za leo. Ee Yesu, ufalme wako utufikie.

 

BABA YETU.

Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe. Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.

Utupe leo mkate wetu wa kila siku. Utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina.

 

SALAMU MARIA.

Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa.

Maria Mtakatifu mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

 

KANUNI YA IMANI.

Nasadiki kwa Mungu Baba mwenyezi. Muumba wa Mbingu na dunia. Na kwa Yesu Kristo Mwanae wa pekee, Bwana wetu. Aliyetungwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akazaliwa na Bikira Maria. Akateswa kwa mamlaka ya Ponsiyo Pilato. Akasulibiwa, akafa, akazikwa, akashukia kuzimu. Siku ya tatu akafufuka katika wafu. Akapaa mbinguni, amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi. Toka huko atakuja tena kuwahukumu wazima na wafu.

Nasadiki kwa Roho Mtakatifu, kanisa takatifu katoliki, ushirika wa watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili na uzima wa milele ijayo. Amina.

 

AMRI ZA MUNGU.

1. Ndimi Bwana Mungu wako, usiabudu Miungu wengine.

2. Usilitaje bure jina la Mungu wako.

3. Shika kitakatifu siku ya Mungu.

4. Waheshimu Baba na Mama upate miaka mingi na heri duniani.

5. Usiue.

6. Usizini.

7. Usiibe.

8. Usiseme uongo.

9. Usitamani mwanamke asiye mke wako.

10. Usitamani mali ya mtu mwingine.

 

AMRI ZA KANISA.

1. Hudhuria misa takatifu, dominika na sikukuu zilizoamriwa.

2. Funga siku ya jumatano ya majivu; usile nyama siku ya ijumaa kuu.

3. Ungama dhambi zako walau mara moja kila mwaka.

4. Pokea Ekaristi takatifu hasa wakati wa Paska.

5. Saidia kanisa katoliki kwa zaka.

6. Shika sheria katoliki za ndoa.

 

Ee Maria Bikira Mtakatifu, Mama wa Mungu na Mama yangu, nawe Mtakatifu Yosefu, Nawe malaika mlinzi wangu, nanyi watakatifu somo wangu, nanyi watakatifu wote, niombeeni nipate kuacha dhambi, nilindeni siku ya leo na siku zote, na saa ya kufa kwangu, Amina.

 

SALA YA IMANI.

Mungu wangu, nasadiki maneno yote. Linayosadiki na linayofundisha Kanisa Katoliki la Roma. Kwani ndiwe uliyetufumbulia hayo. Wala hudanganyiki, wala hudanganyi. Amina.

 

SALA YA MATUMAINI.

Mungu wangu, natumaini kwako, nitapewa kwa njia ya Yesu Kristo. Neema zako hapa duniani, na utukufu mbinguni. Kwani ndiwe uliye agana hayo nasi, nawe mwamini. Amina.

 

SALA YA MAPENDO.

Mungu wangu, nakupenda zaidi ya chochote. Kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na jirani yangu, kama nafsi yangu, kwa ajili yako. Amina.

 

SALA YA KUTUBU.

Mungu wangu nimetubu sana, niliyokosa kwako. Kwani ndiwe mwema, ndiwe nwenye kupendeza. Wachukizwa na dhambi, basi sitaki kukosa tena. Nitafanya kitubio, naomba neema yako, nipate kurudi. Amina.

 

SALA KWA MALAIKA MLINZI.

Malaika mlinzi wangu, unilinde katika hatari zote, za roho na za mwili. Amina.

 

MALAIKA WA BWANA

•Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, Naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.

 

~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

 

•Ndimi mtumishi wa Bwana, Nitendewe ulivyosema.

 

~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

 

•Neno wa Mungu akautwaa mwili, akakaa kwetu.

 

~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

 

Utuombee Mzazi Mtakatifu wa Mungu, tujaliwe ahadi za Kristo.

 

Tuombe:

Tunakuomba Ee Bwana utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya malaika, kwamba Kristo mwanao amejifanya mtu; kwa mateso na msalaba wake, tufikishwe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu, Amina.

 

 

*SALA YA KUOMBA KUWA MKARIMU*

 

■Bwana Yesu, nifundishe kuwa mkarimu;

 

■Nifundishe kukutumiki unavyostahili;

 

■Kutoa bila kuhesabu gharama;

                                                                                                                 

■Kupigana bila kujali ujeruhi;

 

 ■Kujitahidi bila kutafuta pumziko;

 

■Kutumika bila kutafuta tuzo;

 

■Ispokuwa kule kujua nafanya mapenzi yako ......Amina

 

*SALA YA KUMSHUKURU MUNGU*

 

Nakushukuru Ee Mungu kwa ulinzi na baraka zako zote  unazonijalia 

Nakuomba unijalie hekima na busara katika kunena na katika kutenda

unisaidie iliniweze  kuyashinda  maisha  yanayo nisongasonga. Nakuomba unisaidie niweze 

kutimiza malengo yangu na unikinge hatari zote za mwili na za roho katika kuyafikia malengohayo.Usiniache nianguke katika maovu. Uwape mafanikio wote wanaohitaji msaada wako. Nakuomba unijalie kifo chema na uwapokee kwako marehemu wote hasa ndugu zangu. Naomba haya yote kwa njia ya Kristo Bwana wetu..... Amina.🙏

 

 

*Sala kabla ya Kazi.*

 

Uje Roho Mtakatifu, uzienee nyoyo za waumini wako uwatie mapendo yako peleka roho wako vitaumbwa upya na nchi itageuka.

 

*Tuombe.*

 

Ee Mungu uliye fundisha nyoyo za waumini wako, ukiwaletea mwanga wa Roho Mtatifu tunakuomba tuongozwe na yule Roho,tutende yaliyo mema tupate daima na faraja zake.

Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. *Amina.*

 

*Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu.Amina.*

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAHAMU JINSI YA KUOMBA SALA YA VITA

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

SALA KWA AJILI YA KUFUNGULIWA KUTOKA KATIKA NGUVU ZA GIZA

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO

IBADA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA