SIMULIZI ZA KWELI KUHUSU TOHARANI.


SIMULIZI ZA KWELI KUHUSU TOHARANI.

 

✝️ Toharani ni mahali pa mateso, lakini ndani yake kuna furaha na matumaini makubwa ya kumuona Mungu siku moja.

 

✝️ Roho zilizoko Toharani ni tofauti kabisa na sisi tuliokuwa hai angali bado tuko duniani, kwa sababu tunaishi tu bila kuwa na uhakika kama tutamuona Mungu baada ya kufariki.

 

✝️ Kwa mujibu wa Katekisimu ya Kanisa Katoliki inasema: Toharani ni mahali pa Utakaso, ambapo mtu mwenye dhambi ndogo ndogo anapokufa, basi hulazimika kwanza kuingia Toharani kutakaswa kabla ya kwenda Mbinguni.

 

✝️ Hivyo ni jukumu letu la kila siku kama Kanisa linalosafiri hapa duniani, kuwasaidia hawa wenzetu katika sala, Ili wapate neema ya haraka katika kushiriki furaha ya Pasaka huko Mbinguni. Kwani roho zilizoko Toharani, wanahitaji sana sala zetu.

 

*1. MTAKATIFU PADRE PIO*

 

Simulizi hii ni ya kweli iliyotokea kule Italy, linaonesha wazi kwamba, roho zilizoko Toharani daima wanahitaji sana sala zetu Ili watoke huko.

 

Siku moja mnamo mwaka 1920, Mtakatifu Padre Pio alipokuwa akisali katika lofti ya kwaya, ghafla alisikia sauti ya ajabu kutoka kwenye Altare ya Kanisa.

 

Ilikuwa ni sauti ya Candelabra, kijana mdogo sana wa makamo, ikianguka kutoka kwenye Madhabahu kuu. Padre Pio alipomuona, Kijana yule akamwambia:

 

"Baba, ninafanya malipizi yangu hapa Toharani, maana nilikuwa mwanafunzi katika seminari hii. Sasa nahitaji kurekebisha kwa makosa niliyoyafanya wakati nilipokuwa hapa, kwa sababu ya uvivu wangu wa kufanya kazi za Kanisa kwa ulegevu".

 

Pia inasemekana kwamba, kijana huyo alikuwa Toharani takribani miaka 60, na baada ya kuomba maombi kutoka kwa Padre Pio, alipotea na kurudi Toharani.

 

Roho nyingine nyingi sana kutoka Toharani, zinasema kwamba: Baada ya kuomba msaada wa Padre Pio, basi alitumia usiku mzima katika sala akiwaombea. Na hivyo Mungu kupitia sala zake, aliwahurumia na kuwaruhusu kuingia Mbinguni.

 

*2. MTAKATIFU THERESA WA AVILA*

 

Mtakatifu huyu alikuwa ni Mtawa wa Shirika la Wakarmeli, na inasemekana kwamba ndiye Mwanzilishi wa shirika hilo akishirikiana na Mtakatifu Yohane wa Msalaba.

 

Mtakatifu Theresa wa Avila naye alisema kwamba: Baada ya kujua kuwa Padre wake alikuwa amekwisha kufa, basi Mungu akamwambia, Padre huyo atakuwa Toharani hadi Misa itakaposomwa katika Kanisa la nyumba mpya ya Wakarmeli itakayojengwa.

 

Kwa haraka Mtakatifu Theresa alikwenda kwenye eneo la ujenzi na kutafuta wafanyakazi, kwa ajili ya kuanza kazi ya kuinua kuta za Kanisa mara moja.

 

Lakini kwa kuwa iliweza kuchukua muda mrefu kukamilika, basi aliomba ruhusa kutoka kwa Askofu kwa ajili ya kujenga Kanisa la muda mfupi.

 

Kanisa lilipokamilika, Misa iliadhimishwa hapo. Na wakati alipokuwa anapokea Sakramenti ya Ekaristi Takatifu, Mtakatifu Theresa aliweza kuona maono ya Padre yule akimshukuru kwa neema alizozipata  kwake kabla ya kuingia katika Ufalme wa Mungu.

 

*3. MTAKATIFU ELIZABETH WA URENO*

 

Mtakatifu huyu ambaye alitawala Ureno kama Malkia wa nchi yake, alikuwa na binti aliyempenda sana aitwaye Constance.

 

Mtoto huyu mdogo alikufa ghafla baada ya kuolewa, na kusababisha Malkia Elizabeth na Mumewe kupata huzuni nyingi juu ya kifo chake.

 

Siku moja Hermit alimwendea Malkia Elizabeth alipokuwa anasali, akamwambia habari ya kushtusha sana kwamba, Constance alimtokea akimuomba achukue ujumbe kutoka kwa mama yake huku akimueleza kuwa, sehemu aliko kule Toharani anateseka sana, na angeendelea kuwa huko kwa muda mrefu zaidi.

 

Basi baada ya maelezo hayo, wakaamua kuweka Misa Takatifu kila siku kwa ajili yake. Naye Constance kupitia maombezi ya Malkia Elizabeth na watu wake wa karibu, aliweza kupata huruma ya Mungu na kuruhusiwa kuingia Mbinguni.

 

✝️ Ndugu yangu, hizi ni simulizi chache tu nimekuandalia ili uone Toharani ni sehemu pa namna gani.

 

✝️ Kwani Toharani haina utofauti na Jehanamu, kwa sababu zote zina moto. Lakini uzuri ni kwamba, moto wa kule Toharani uko kwa ajili ya kuzitakasa roho kabla ya kuingia Mbinguni.

 

✝️ Kwahiyo Toharani sio mahali pa mchezo, na ndio maana Mama Kanisa ameweka mwezi huu wote wa Novemba kwa ajili ya kuziombea Roho hizo zilizoko Toharani, ili kupitia sala zetu, wapate neema ya haraka ya kutoka huko.

 

✝️ Kipindi hichi cha Novemba, sio tu kwa ajili ya kuziombea roho zinazoteseka Toharani, bali pia ni kwa ajili yetu wenyewe, tujitafakari baada ya maisha ya hapa duniani tutakuwa wapi.

 

✝️ Hivi ushawahi kujiuliza kwanini bado unaishi? Najua utakuwa hujui, ila ukweli ni kwamba unaishi ili kwa sababu utumie muda wako vizuri katika kutenda mema na kumtumikia Mungu siku zote, na ndio maana bado uko hai.

 

✝️ Siku moja nlipokuwa Kwenye Misa nilimsikia Padre mmoja katika Mahubiri yake akisema kwamba:

 

✝️ Watu wema na wabaya hufa kwa sababu, wale waliokuwa wema wasiendelee kubaki duniani wasije kuanguka dhambini na kukosa Ufalme wa Mbingu.

 

✝️ Pia hata wale waliokuwa wabaya hufa mapema, ili wasisababishe wale waliokuwa wema wakatenda dhambi na kupotea kwenye ziwa la moto wa milele.

 

✝️ Hivyo kwa kuwa sisi bado tunaishi, ni wazi kwamba tuko katikati yaani sio watu wema sana na wala sio wabaya mno. Kwahiyo tunaishi ili kujenga maisha yetu ya baadae baada ya kuondoka hapa ulimwenguni.

 

✝️ Basi pumzi tuliyonayo tuitumie vizuri katika kutenda mema, na sio kufanya mambo ya anasa, zinaa, ulevi na yote yahusuyo dunia.

 

✝️ Ni heri kufanya matendo mema hapa duniani, hata kama utakufa na usimuone Mungu, hiyo haina shida. Kuliko ufe katika hali ya dhambi kubwa huku ukisema hakuna Mungu, halafu baadae unakufa na ukamuona Mungu. Sijui itakuwaje.

 

✝️ Hivyo mwezi huu ni mwezi wa kujitafakari juu ya maisha yetu wenyewe, kama kuna sehemu tumekosea tujirekebishe. Pia tusisahau kuwaombea na wenzetu walioko Toharani, maana walikuwa kama sisi tulivyo, na siku moja na sisi tutakuwa kama wao.

 

✝️ Sote tu marehemu watarajiwa, tuishi vizuri katika Upendo na wenzetu, ili tutakapokufa hapa dunia tuache alama nzuri ya kuigwa na siku moja tukapokee tuzo ya Utakatifu huko Mbinguni.

 


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA

ROZARI YA KUWAOMBEA MAREHEMU TOHARANI

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

IBADA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

TAMBUA UMUHIMU WA KUOMBEA MIMBA KWA MAMA MJAMZITO

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO