MKAKATI WA WACHAWI KUKUZA NA KUENEZA UCHAWI


 

MKAKATI WA WACHAWI KUKUZA NA KUENEZA UCHAWI

Tumsifu Yesu Kristo.

Ndugu zangu katika Kristu, Katika makala hii napenda kuwashirikisha mkakati wa kukuza na kueneza uchawi.

Unaweza usielewe, lakini tunakoelekea tutegemee kuwa na wachawi wengi zaidi, kwa sababu wachawi wamegundua njia bora na nzuri ya kueneza uchawi wao ni kuwafundisha watoto wadogo, na kuwalisha viapo katika Ulimwengu wa giza kiasi kwamba hata mtoto akijitambua anashindwa kujitoa kabisa.

Watoto wafuatao wapendwa sana kufundishwa uchawi.

1.    Watoto wa wachawi wenyewe

2.    Watoto Yatima

3.    Watoto ambao wazazi wao wanamafarakano

4.    Watoto ambao ndugu zao ni wachawi

5.    Watoto ambao marafiki na majirani zao ni wachawi na ni rafiki wa familia zao. (kuozeshana watoto wao kwa wao kwa lengo la kukuza uchawi wao.)

 

·         Watoto hawa huibiwa nafsi zao, na nafsi zao hizo upelekwa kufundishwa uchawi kwa muda mrefu, na mtoto aliyeibiwa nafsi akilala usiku uota mambo mazito akifanya ikiwa ni pamoja na kunywa damu, kula nyama mbichi, kushiriki vikao na watu waliovaa nguo nyekundu au nyeusi, katika hali hiyo atafundishwa mambo mengi katika ulimwengu wa roho kwa kutumia nafsi yake, na hakiisha komaa nafsi ile uachiwa kurudi katika mwili wake ikiwa na uzoefu wa hali ya juu, hapo hapo mtu huyu uanza kutenda kwa uhalisia wake matendo ya kichawi, kuchezea wenzake kwa nguvu za giza n.k na katika hali yote atakuwa ni mwenye furaha.

Kitendo cha wachawi pia kuozeshana watoto wao ni mkakati wa kukuza na kurisisha uchawi wao kizazi hadi kizazi bila shida yeyote.

·         Watoto yatima pia wanapata changamoto hii kwa sababu wachawi wanatambua wazi kuwa mtoto huyu sio rahisi kupata msaada wa kiroho hivyo, ni rahisi wao kumtumia watakavyo, na mtoto huyu uweza kukataa shule kabisa kama anasoma, na hapo uweza kuota mambo makubwa kumbe anafundishwa na akikomaa uona raha na kuendelea na kazi yake ya uchawi.

Tatizo kubwa linalosababisha ongezeko la uchawi pia ni familia nyingi hazisali, na familia nyingi uamini na kutegemea nguvu za giza.

·         Ndugu zangu kazi ya Mchawi ni kuharibu na furaha ya mchawi ni kukuona wewe unateseka, kwa lugha fupi, mtu yeyote anayefurahia wewe unavyoteseka mtu huyo ni mchawi wako, kwa sababu angeweza kukufanya wewe uteseke angefanya ila kwa kuwa awezi na sasa anafurahi mateso yako huyo hana tofauti yeyote na mchawi tu.

·         Ukitaka kujua uchawi unaongezeka unaweza kufanya utafiti kwa watoto wa darasa la chekechea, la kwanza na la pili, watoto hawa ukijiusisha na kuwa rafiki yao mwema na kuongea nao kwa akili utaona watoto wenye kutoka familia za kichawi, yaani watoto walio wachawi watakavyo kusimlia mambo ya nyumbani kwao kwa raha kubwa, jinsi anavyologa yeye na Bibi yake au Babu yake historia zingine unaweza cheka kidogo.

Lakini ndivyo ilivyo. Hawa watoto ndio tunategemea kuwa viongozi wetu wa baadaye maana baadhi ya wachawi hujua umuhimu wa elimu lakini wengine hawajui kabisa na hao ni wengi, ukikuta mchawi mwenye kupenda elimu atawaongozea darasani na walimu walio wachawi wote watampenda sana, hivyo tutegemee kwa stahili hii kupata viongozi wachawi au washirikina mno. Ili kuzuia ongezeko la uchawi tufanyeje?

Ø  Tunatakiwa kuwalea watoto wetu kwa kuwaelekeza ili wamjue Mungu, wampende, watenge muda wa kuongea naye.

Ø  Kuwaombea watoto wetu kwa kuwatenganisha na maagano yote toka mti wa familia ili yasiweze kuwasumbua katika makuzi yao.

Ø  Kuzifanya nyumba zetu kuwa kanisa dogo, yaani kusali bila kuchoka ndani ya familia.

Ø  Kuongea na watoto wetu, kuna watoto wanateseka sana, wanashindwa wamshirikishe nani ili kupata msaada. Tutenge muda wa kuongea na watoto hawa na kuwashirikisha upendo wa Mungu.

Hebu tujiulize swali, je mchawi pia husali?

Jibu ni ndiyo, wachawi walio wajanja uigiza kusali, na nikwanza kanisani, upenda kujionyesha sana kuwa wao ni wacha Mungu sana, kwenye vikundi vya sala wapo, lakini uchagua vikundi, vile vilivyo dhaifu ujiunga navyo. Wachawi wa namna hii ni rahisi sana kuwakomboa maana wanapenda kusali wakiwa na mikoba yao, ikitokea siku wakakutana na nguvu ya Mungu ukombolewa kabisa.

Ndugu zangu katika Kristu, tuache ushirikina, Tusali na tuwafundishe watoto wetu kumjua, kumpenda Mungu na kumtumikia, kwa kufanya hivi tutapunguza sana, ongezeko la wachawi ndani ya koo zetu.

Mungu atubariki sana.

Unaweza kutazama video hizi ili kuzama ni mbinu gani Wachawi utumia kwa watoto ili kueneza uchawi wao.

Tazama binti huyu aliyeandaliwa kuwa Mchawi.


SHEMU YA PILI YA VIDEO YA BINTI ALIYEANDALIWA KUWA MCHAWI.


SHEMU YA TATU YA VIDEO YA BINTI ALIYEANDALIWA KUWA MCHAWI.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAHAMU JINSI YA KUOMBA SALA YA VITA

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

SALA KWA AJILI YA KUFUNGULIWA KUTOKA KATIKA NGUVU ZA GIZA

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO

IBADA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA