MADHARA YA VIONGOZI WASHIRIKINA


 

MADHARA YA VIONGOZI WASHIRIKINA

Tumsifu Yesu Kristo.

Ndugu zangu wote tunajua maana ya madhara, madhara ni uharibifu au athari mbaya tunaweza kuziona baada ya kufanya kitu Fulani na ushirikina ni wazo ambalo halina sababu yenye msingi katika maarifa au mang’amuzi na neno ili hutumiwa kwa kutaja imani ambazo hazina msingi au tunaweza kusema ushirikina ni sayansi iliyotolewa kwa uhusiano kati ya viumbe visivyo hai na wanadamu, uchawi na ushirikina yanaweza kufanana, ushirikina ni kitendo cha kwenda kutafuta msaada wa kiroho au kimwili katika Mamlaka ya giza, namaanisha kwa shetani na mapepo, majini yake yanayofanya kazi kupitia watu wanaoitwa waganga au wachawi.

Hivyo leo tuangalie watu hawa ambao ni viongozi wetu na niwashirikina yaani katika utendaji wao wa kazi wanawategemea waganga au wachawi, watu wa namna hii hawawezi kuleta maendeleo katika eneo lao la kazi kwa sababu ya tumia nguvu za giza zaidi wanaweza kusababisha mambo yafuatayo katika maeneo yao ya kazi:-

1.   MIGOGORO

Tukumbuke washirikina ni watu wanaofanya kazi zao au kutimiza wajibu wao kwa kutumia nguvu za giza ambazo zimetengenezwa katika maumbo mbalimbali kama vile pete, irizi, cheni n.k au manuizo, kazi zote hizi usimamiwa na mapepo hivyo kama wewe ni mtu wa sala sana, watu hawa mtapambana nao na watakuchukia sana na kutengeneza migogoro isiyo ya lazima.

 

2.   MAENDELEO

Viongozi wa namna hii hawawezi kuleta maendeleo hata mara moja katika kipindi chao chote cha utawala, maana wanaamini wapo hapo kwa msaada wa nguvu za giza na ni watu hatari sana, wasio na utu hata kidogo maana wanaongozwa na mapepo, au wanaamini ulinzi wa nguvu za giza.

 

3.   KUSALI

Ni watu ambao hawapendi kusali kabisa au kushiriki matukio ya kiibada, hata ruhusa zao ni shida, na wanapenda sana kutukuzwa, kuheshimiwa hata pasipo stahili heshima.

 

4.   KUONGELEA NGUVU ZA GIZA

Watu hawa hawapendi kabisa kusikia mjadala wa kulaani nguvu za giza, zaidi utasikia wakisisitiza hakuna ushirikina, hakuna uchawi na hata sala zao ni za kujionyesha kuwa wanasali sana, kuficha uovu wao lakini nyuma ya pazia ni washirikina wa ajabu.

 

5.   USHAURI WAO

Ushauri wao unategemea na wewe ulivyo, ukiwa ni mtu wa dini, kama ni boss wako atajifanya kukushauri sawa sawa na ulekeo wako kuwa umtegemee Mungu, kama ni mshirika mwenzake atakuongoza kwa mtaalamu mwingine zaidi.

 

6.   MAHUSIANO SEHEMU YA KAZI

Kiongozi mshirikina uimarisha mahusiano makubwa na washirikina wenzake, wachawi wenzake kwa kila jambo. Awawapendi kabisa watu wanaosalisali, na wanateteana sana katika maeneo ya kazi hata boss akija na wazo la kipuuzi, wazo hili litapita kwa asilimia zote, sio wa kweli.

 

7.   MWISHO WAO.

Viongozi wa namna hii hawamalizi vizuri uongozi wao au maisha yao, maana kwa ujeuri wao watakuwa wameathiri watu wengi katika uongozi wao kwa kuwanyanyasa, hivyo wengine upata malipo yao hapa hapa.

 

HATUA ZA KUCHUKUA KUPAMBANA NA VIONGOZI WASHIRIKINA

 

·         Kumbuka kuwa wewe ni mwanadamu uliumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, kumbuka pia kuwa umepewa mamlaka na Mungu ya kutawala viumbe vyote na kuvitiisha, kumbuka pia mapepo, majini na nguvu zingine zote za kichawi zipo chini ya mamlaka yako kwa jina la Yesu.

 

·         Vaa silaa zote za vita  kama ilivyoandikwa Waefeso 6:10-20, tumia mamlaka hayo kumfunga boss wako Mshirikina, sambaratisha na nguvu yake yote aliyoweka kwenye Ofisi yake au anayotembea nayo, ukorofi wake wote mbele yako ushughulikiye kwa nguvu ya maombi, akikufokea wala usiangaike kumjibu kimwili bali mjibu kiroho, funga hiyo roho inayokuchukia kwa jina la Yesu, hata mkianza kikao kitawale kikao hicho kwa kusema kwa Imani kuu, (Nakifunga kikao hiki kwa jina la Yesu mwovu yeyote hana Mamlaka nacho) jitahidi uwe mtu wa sala daima, na hapa utaona kiongozi wake anabadilika ghafla na kukupenda, lakini pia kutenda haki na kuleta maendeleo lakini ikishindikana kuwa hivyo inakuwa kinyume chake kwa maana anaweza kufukuzwa kazi, kushushwa cheo au kuhamishwa eneo ulipo na mambo yote haya yanatokea automatic yaani kwa mapenzi ya Mungu.

 

·         Viongozi hawa upenda sifa sana hata wasizositahili wewe msifu tu, mtapatana, wala usijenge nao mazoea hadi kwenye familia yako, wanawivu sana wa maendeleo, kuwazoesha nyumbani au kuwasimlia maendeleo yako ni hatari sana, hivyo acha kuwasimlia maendeleo yako.

 

Mwisho na muhimu dumu katika sala, wataomba uhamisho wenyewe au kujihudhuru nafasi zao na wewe daima ndio mshindi.

 

 

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAHAMU JINSI YA KUOMBA SALA YA VITA

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

SALA KWA AJILI YA KUFUNGULIWA KUTOKA KATIKA NGUVU ZA GIZA

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO

IBADA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA