IJUE NGUVU YA MSAMAHA

 


IJUE NGUVU YA MSAMAHA TOKA MAKALA HII ILIYOANDALIWA

NA MTUMISHI JULIUS MMBAGA

 

Ndugu Msomaji leo nataka ujue nguvu ya msahama katika kufanikiwa katika safari ya maisha yako.

Sisi kama Wakristo tumekuwa kukisali sala ya Baba Yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, ufalme wako ufike utakalo lifanyike duniani kama mbinguni, utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu kama tunavyo wasamehe na sisi waliotukosea, usitutie katika vishawishi bali utuokoe maovuni. Amina.

Salah hii ya Baba yetu tunaisali sana., je ni kweli tunawasamehe wenzetu waliotukosea hebu soma Mt. 6-7-15 na ni vema uelewe wazi kuwa :-

1.    Tunafurahia msamaha wa Mungu kwa kiwango kile ambacho sisi pia tupo tayari kuwasamehe wengine.

2.    Hivyo kila mtu ambaye hujamsamehe maishani mwako ni ushahidi wa kuwepo kwa dhambi zako katika maisha yako ambazo Mungu hajasamehe.

3.    Kutosamehe ni kitu kigumu sana lakini ni chenye madhara kwa sasa na baadaye, baadhi ya watu wanaugua magonjwa ambayo tiba yake ni kusamehe tu, unakutana na mtu anaugonjwa wa shinikizo la damu, ana ugonjwa wa hasira na kila siku anapanga kulipiza kisasi, anatamani kujiua au kuuwa, anatamani kusababisha madhara makubwa, kwa sababu tu ameshindwa kusamehe, mpaka anakuwa na magonjwa kwasababu ya ugumu wa moyo wake, na hii inasababisha roho chafu, roho za kiburi, roho za kisasi.

Siku moja nilikuwa natoa huduma, na baada ya huduma nilimsihi aliyekuwa mgonjwa kuwasamehe watesi wake, naye alikataa kabisa, baada ya ushauri wa kutosha alikubali kuachia msamaha, basi alipofumbua kinywa chake kutangaza msamaha, aliruka juu na kudondoka chini na kuviringika kama tairi la gari na mwisho alinyooka na kupiga kelele na hapo akaweza kuachia msamaha na kupona kabisa, na ile nguvu kwa nguvu ya msamaha ilitoweka kabisa na alijisikia mwili mwepesi.

4.     Hebu tujitafakari sote sisi kama wakristo usipokubali kusamehe ni dhahiri nawe hautaki kusamehewa dhambi zako, na usiposamehewa dhambi zako, utaurithije uzima wa milele maana hakuna kinyoge kitaingia kule.

 

5.    Kama uwezi kusamehe ni muhimu kwamba neema ya kusamehe kila unaposimama kusali, kama una neno na mtu msamehe na wewe usamehewe maana usiposamehe hata maombi yako hayatasikilizwa na Mungu hebu soma Mark 11:25-26 inasema hivi (Mnaposimama kusali, msameheni kila mtu aliyewakosea chochote, ili Baba yenu aliye mbinguni awasamehe nyinyi makosa yenu) hivyo kama utaamua kukomaa na kutosamehe watu makosa yao basi ujue hata wewe hautasamehewa na usiposamehewa huwezi kusikilizwa maana Mungu hayasikilizi maombi ya mwenye dhambi soma Yohana 9:31 (Twajua kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, bali mtu akiwa ni mcha Mungu na kuyafanya mapenzi yake, humsikia huyo) Zaburi 66:18 (Kama ningelinua maovu moyoni mwenyezi Mungu hangalinisikiliza)

 

6.    Nguvu ya kusamehe tunakuwa nayo katika somo la utoaji ukisoma Mathayo 5:23 -26 (Patana na mshitaki wako upesi mkiwa bado njiani kwenda mahakamani. La sivyo, Mshitaki wako atakukabidhi kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa Askari, nawe utafungwa gerezani, kusamehe pia ni chanzo cha kiburi, wewe unakuwa na kiburi cha kuomba msamaha kwa jambo dogo, ambalo lingemalizika kwa mazungumzo tu, lakini kiburi na hatimaye ukifikishwa mahakama sharia uchukua mkondo wake na hatimaye waweza kufungwa kabisa.

 

7.    Watu wengi wanasali, wanamuomba Mungu usiku na mchana moambi yao, kumbe Mungu amekwisha wajibu maombi yao, na maombi yao yako hewani yanazunguka zunguka tu, kwa sababu haya pa kuingia, mioyo yao imejaha visasi, mioyo yao imejaa kutosamehe, imejaa mahangaiko wabaki kulalamika Mungu hawasikii wakiomba na hatimaye wanakuwa washirikina hodari maana huko na kutosamehe kwao vinapatana kabisa.

 

8.    Tukumbuke kabisa kutosamehe kwako kunaathiri mpaka utoaji wako wa sadaka kwa Mungu soma Luka 17:3-4 (Jihadhari kama ndugu yako akikukosea, muonye, akitubu msamehe na akikukosea mara saba kwa sikou na kila mara akirudi kwako akisema, nimetubu, lazima umsamehe)  Hivyo unaweza kuona neno la Mungu linasisitiza kusamehe maana ushindi wa maombi yako na mafanikio yako huko hapo, yatupasa tujilinde ili kule kukosewa kwetu kusiwe sababu ya kuyaharibu kabisa maisha yetu, tuombane msamaha tuache kiburi.

 

Kusamehe hakuna ukomo, Mathayo 18:21-22 (Kisha Petro akamwendea Yesu, Je, ndugu yangu akinikosea nimsamehe mara ngapi?  Mara saba? Yesu akamjibu, "sisemi mara saba tu, bali sabini mara saba) Utaona hesabu hii kwa elimu ya Petro ilikuwa hesabu kubwa mno hii inatupasa kutambua wazi kusamehe hakuna ukomo na kusamehe sio kuwa mjinga.

 

Mateso mengi ambayo watu wanapitia maishani kwa sababu hawapo tayari kusamehe, kutosamehe kunatoa nguvu kwa watesaji wako na hapa tusome Mathayo 18:32-35 (Hapo yule bwana alimuita huyo mtumishi akamwambia, wewe ni mtumishi mbaya sana! Uliniomba, name nikakusamehe deni lako lote, Je, haikukupasa nawe kumhurumia mtumishi mwenzako kama nilivyo kuhurumia? Basi, huyo Bwana alikasirika sana, akamtoa huyo mtumishi aadhibiwe mpaka hapo atakapolipa deni lote, na Baba yangu aliyeko mbinguni atawafanyieni hivyo hivyo kama kila mmoja wenu hatomsamehe ndugu yake kwa moyo wake wote.

 

Hapo tunaona Yesu amekuwa wazi mno na kutuonyesha madhara ya kutosamehe, Ndugu yangu sisi tuliosamehewa na Bwana nasi tusamehe na katika kusamehe tunapokea neema kubwa sana na maombi yetu yanajibiwa, hebu tukasome

Efeso 4:31-32, Wakolosai 3:12-13

Warumi 12: 7-21 (Msimlipe mtu ovu kwa ovu) ushindeni ubaya kwa wema.

Ndugu zangu hata kama una hasira Efeso 4:26-27 inasema Muwe na hasira ila msitende dhambi, jua lisichwe na uchungu bado haujawatoka wala msimpe Ibilisi nafasi.

Mungu atubariki na kutujalia neema ya kusamehe katika maisha yetu.

 

Imeandaliwa na

Mtumishi: Julius Mmbaga

0766500747


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA

ROZARI YA KUWAOMBEA MAREHEMU TOHARANI

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

IBADA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

TAMBUA UMUHIMU WA KUOMBEA MIMBA KWA MAMA MJAMZITO

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO