HADITHI YA KWELI KUHUSU MAREHEMU WALIOKO TOHARANI

 


HADITHI YA KWELI KUHUSU MAREHEMU WALIOKO TOHARANI.

 

Siku moja huko San Giovanni Rotondo, Padre Pio pamoja na Watawa wenzake walikuwa wanasali, mara walisikia sauti za ajabu zikitoka kwa Kasisi. Mmoja wa Mafrateli alisikika akisema:

 

"Tulisikia sauti za ajabu huku zikiwa zinaimba kwa mtiririko mzuri, lakini cha kushangaza hakuna aliyejua chanzo cha sauti hizo zilikuwa ni nini".

 

Wakati hayo yakiendelea, Padre Pio alikuwa amezama sana katika maombi, ndipo Mtawa mmoja akamkaribia ili kumuuliza kama kweli anajua uimbaji huo ulikuwa unatoka wapi.

 

Wakati alipomgusa, Padre Pio alishtuka kana kwamba ametoka katika usingizi mzito sana, kisha akajibu:

 

"Mbona nyote mmeshangaa? Hizo mnazozisikia ni sauti za Malaika zikiimba, huku wakizitoa roho kutoka Toharani na kuzipeleka Mbinguni".

 

Padre Pio hakuweza tu kusikia, bali pia aliweza kuona kwa macho ya rohoni kila kitu kilichokuwa kinatendeka muda ule.

 

Pia nyakati zingine, alipewa zawadi ya kujua hali ya milele kwa wale wanaokufa. Na inasemekana kwamba:

 

Siku moja alitembelewa na Mjane mmoja ambaye Mume wake alijiua, aliyemuuliza kuhusu roho ya Mume wake na Padre Pio akamjibu:

 

"Ukweli Mume wako ameokoka, kati ya daraja na moto alimojitupa, kwa kuwa alitubu".

 

Basi zawadi za Padre Pio zisizokuwa za kawaida, hazikuja kwa urahisi. Daima alitambua maisha yake ya mateso makali, ikiwemo kubeba Majeraha ya Stigmata (yaani Madonda ya Yesu) kwa zaidi ya miaka 50, kwa ajili ya marehemu Toharani.

 

Katika mateso yake, Padre Pio alikuwa na Ibada maalumu kwa roho zilizomo Toharani. Mapema katika Ukuhani wake, alimwandikia Mkurugenzi wake wa kiroho kuwa:

 

"Tamaa hii imekua mara kwa mara moyoni mwangu, hadi sasa nimekuwa na shauku kubwa kwa ajili ya hiyo.

 

Kwani nilitoa dhabihu hii kwa Bwana, nikimsihi aniweke juu yangu adhabu ambazo zimetayarishwa kwa ajili ya wenye dhambi na roho zilizomo Toharani, na kuzidisha juu yangu adhabu hizo hata mara mia, Ili roho yenye dhambi ikoke na kuachilia haraka roho zinazoteseka Toharani".

 

Padre anaendelea kusema kwamba:

 

"Mateso yalipozidi bila faraja, ilikuwa furaha yake kubwa, kwa sababu yaliyafanya maumivu ya Yesu kuwa mepesi".

 

Basi ndugu zangu, kesho tunapojiandaa kushiriki sherehe ya Kristo Mfalme, tusisahau kuwaombea ndugu zetu marehemu walioko Toharani.

 

Kwani Bwana Yesu mwenyewe aliahidi kwamba: "Katika sherehe hii, yeyote atakayesali kwa ajili ya kuwaombea marehemu wake, basi atazifungua roho hizo kutoka kwenye kifungo cha mateso na kuwaingiza katika Ufalme wake wa milele, kama tu mtu huyo atasali kwa imani na kupokea Ekaristi Takatifu."

 

*RAHA YA MILELE UWAPE EE BWANA...*

 


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA

ROZARI YA KUWAOMBEA MAREHEMU TOHARANI

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

IBADA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

TAMBUA UMUHIMU WA KUOMBEA MIMBA KWA MAMA MJAMZITO

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO