ELIMU NA NGUVU ZA GIZA

 


ELIMU NA NGUVU ZA GIZA

Tumsifu Yesu Kristo
Ndugu zangu wapendwa katika Kristo Yesu, leo napenda kuwashirikisha changamoto kubwa ambayo inawapata baadhi ya watoto katika elimu nasi tunaona ni kitu cha kawaida tu.

1.    Mtoto kukataa shule kabisa bila sababu za msingi.

Tumeona baadhi ya watoto wengine wanakataa shule kabisa hasa wakati wanapoelekea madarasa ya mitihani au kukaribia madarasa ya mitihani, na hali hiyo inaonekana katika jamii kama kitu cha kawaida, nakusema mtoto huyu kakataa shule. Hapana, baadhi ya watoto wanasongwa na nguvu za giza na kujikuta hawataki shule kabisa na hatimaye uacha kabisa masomo. Na hata akiacha shule hawezi kufanya kitu chochote cha maana kwa sababu nguvu iliyopo ndani yake bado inamdhibiti na kukamata mafanikio yake. Mtoto wa hivi akikutana na nguvu ya Mungu atapenda shule na kurudi darasani na kuendelea na masomo kama kawaida.

 

2.    Mtoto kuugua macho hasa wakati wa mitihani

Kuna watoto wanapata shida kubwa ya macho hasa wanapoingia madarasa ya mitihani na akitoka darasa hili maana yake akilivuka darasa hilo na macho yake upona kabisa, anaweza kuhisi kama mchanga kwenye macho, macho huvuta kila anaposoma, hatimaye huwa mzembe kusoma au kujisomea na kusababisha kufeli au wakati wa mitihani haoni maswali kabisa. Mfano halisi siku moja jioni alikuja binti wa kidato cha pili nyumbani kwangu jioni na mzazi wake, na kesi yake kubwa ni tatizo lililomkumba katika chumba cha mtihani akadai alipogawiwa mtihani wake haukua na maswali na hata alipobadilishwa, hakuweza kuona maswali yeyote kwa mitihani yote miwili na bado mitihani ilikuwa inaendelea ya kidato cha pili.

Binti huyu nilimuomba tusali naye pamoja na baada ya kusali, nguvu ya kichawi ililipuka ndani yake na kudai hawataki haendelee na masomo, lakini baada ya maombi ilimtoka na kesho yake aliweza kuona mitihani yake yote vizuri na kuifanya vema.

 

3.    Mtoto kupata zero au kufeli kabisa.

Kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya watoto wenye akili nje ya darasa, lakini wanapoingia ndani ya darasa hufanya vibaya sana katika masomo yao, hata mkimtazama kwa kumpa mazoezi ya kawaida nje ya darasa unaweza kujiuliza maswali ya kwanini mtoto huyu anapata zero na usipate majibu yake. Kumbe anakamatwa ufahamu wake katika mitihani na nguvu ya giza ndiyo sababu anafeli, kuna roho inamvaa wakati wa mitihani na kumfanyia mitihani hiyo, hivyo hivyo na kwa kuwa familia nayo haina tabia ya kusali, mtoto huyu ataonekana mjinga na hawezi kuendelea na shule tena, hivyo safari yake ya elimu hukomea hapo hapo. Nitatoa mfano kwa watoto wawili mapacha, watoto hawa walikuwa ni mapacha wa kike na wa kiume na wazazi wao wote ni waalimu, watoto hawa walionekana kufanya vibaya sana darasani licha ya juhudi zote za waalimu wao na wazazi wao na viboko vya kutosha bado wote walikuwa wa mwisho darasani kwa kufuatana, walipoingia darasa la saba, wazazi kwakujua uwezo wao waliwarudisha darasa la tano na kuwapeleka private school, bado huko walikuwa wa mwisho darasani. Basi wazazi walipoingia kwenye maombi, watoto wale wote walikombolewa akili zao na mmoja kati yao alikuwa mateka kuzimu kwa miaka nane, hivyo watoto hawa walikombolewa wakiwa tena wamefika darasa la sita kuelekea la saba, walipambana kusoma kwa bidii na walifanya vizuri katika elimu yao,  mpaka ninapoandika makala hii wakike yuko chuo mwaka wa pili na wakiume anaingia kidato cha sita na wote wako huru na wanaendelea vema kabisa na masomo yao.

 

4.    Mtoto kuumwa kichwa kwa maumivu makali sana.

Kuna watoto wamekuwa wakiugua sana na hasa kichwa wapoingia madarasa ya mitihani au wanaingia kwenye chumba cha mitihani, wakitoka kwenye chumba cha mitihani wanapona  au wakivuka darasa la mitihani wanapona kabisa, mtoto wa namna hii anahitaji msaada wa maombi ili nguvu inayoweka makao katika kichwa chake imwacha huru kabisa  ili aweze kuendelea na masomo yake vema kabisa, na kama familia inasali kweli inaweza kumsaidia vema.

 

5.    Kuugua ugua wakati wa mitihani.

Baadhi ya watoto wakati wa mitihani ndio muda wake wa kuuguaugua, kila leo yuko hosiptali, wengine inafikia hatua ya kuhairisha kufanya mitihani kwa sababu ya ugonjwa, kila inapokaribia mitihani ni mgonjwa, mitihani ikipita hupona kabisa, na hatimaye kutokana na changamoto hiyo mtoto huacha shule nasi wazazi huona kuwa ni poa tu.

 

6.    Kusinzia darasani wakati mwalimu anafundisha

Baadhi ya watoto wanatabia ya kusinzia darasani, wakati mwalimu anapofundisha na anasinzia ili asiweze kumsikiliza mwalimu na matokeo yake ni kufeli mitihani, sio kusinzia darasani hata wakati wa kujisomea, akiingia chumba cha kujisomea usinzia mwanzo hadi mwisho, katika hali hii mtoto hawezi kufaulu, kafungwa na anahitaji msaada wa maombi ili kubomoa ngome hiyo, hivyo kama familia inasali vizuri hali hii hutoweka kabisa.

 

7.    Ukiziwi wa kutengeneza.

Watoto wengi waliopata ukiziwi ambao umejitokeza akiwa shule, anaweza kupona kwa asilimia 100% kwa maombi tu, na watoto hawa wanafanywa viziwi ili waweze kufeli mitihani yao, wewe mzazi, umezaa watoto wazima kabisa, ghafla mwanao anakuwa kiziwi wala hushangai, unaridhika tu na matokeo yake mtoto huyo ufeli kabisa mitihani yake kwa sababu ya kutosikia kile mwalimu anachofundisha. Watoto wa hivi nimekutana nao katika maombi na wamepona kabisa.

 

8.    Mwili wa mtoto kukaliwa na nafsi nyingi.

Kuna watoto wengine unafundisha darasani na wewe unaona unamfundisha mtoto kamili, kumbe sio kweli, unamfundisha Bibi yake au Babu yake au kitu kingine na mtoto halisi hayupo hapo, yuko kwingine anafundishwa uchawi, nah ii ni mara chache kugundua ni kwa neema tu. Siku moja nikiwa darasani niliguswa kuwaambia wanafunzi wapige makofi ya kibunge matatu, walipopiga tu yale makofi matatu, niliona mtoto mmoja yuko tofauti kama ana nguvu flani na nilichofanya niliomba darasa zima makofi haya ya kupiga juu ya dawati yaendelee, wakati wakiendelea yule mtoto aliteseka sana, niliondoka darasani huku nikiwataka wanafunzi waendelee kupiga makofi, ile napiga hatua chache, yule mwanafunzi darasani alianza kupiga kelele, nilirudi na kuwaomba wenzake wamtoe nje, nilipomshika mkono yule Bibi wa kichawi aliyekuwa kavaa mwili wa mtoto, alianza kupiga kelele na kusema nimekoma, naomba msaada name nilitaka kuvua vema. Binti halisi yuko wapi, ndipo alisema binti halisi yuko makaburini akifundishwa uchawi, yule Bibi alieleza binti alipokuwa na kazi aliyokuwa anafanya huko na alieleza wazi kuwa toka mwezi January au hiyo Mei mtoto halisi hajawai kukanyaga darasani, ndipo nilipomuita mtoto yule kwa Jina la Yesu kwa nguvu naye alikuja katika mwili wake na kunieleza kuwa kila alipotoka nyumbani tu Bibi yake alimchukua na kumpeleka kumfundisha uchawi, na yeye hurudi darasani kukaa  nafsi yake, Binti huyo alikombolewa, japo alipoingia darasa la sita walimtolesha kabisa na wala hakumaliza shule. Hivyo elimu yake yote iliishia hapo.

 

9.    Kutetemeka wakati wa mitihani, mikono kujaa maji, kizunguzungu, mkono kuwa mzito.

Hizo zote ni dalili za nguvu za giza na dawa kubwa ni maombi tu.

TAZAMA VIDEO HII KUJIFUNZA ZAIDI NGUVU ZA GIZA ZINAVYOFANYA KAZI KUBWA KATIKA ELIMU KUPITIA ULIMWENGU WA ROHO



 

10. Ufaulu wa kipepo au nguvu za giza.

Baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakitumia nguvu za giza katika mitihani yao kwa kuiba akili za watoto wenzao wenye uwezo na kuzitumia darasani, na maendeleo ya watoto wahusika yanaporomoka kabisa. Na ili mtoto aliyeibiwa akili aweze kufanya vizuri ni lazimi afunguliwe na akili zake zikombolewe kwa nguvu ya jina la Yesu.

 

Basi kwa namna ya pekee niwashukuru wote kwa kusoma viashiria vya nguvu za giza katika elimu na dawa ya viashiria vyote ni kusali kwa bidii na mtoto kupata maombi ya kufunguliwa.

Baadhi ya wazazi waliogundua nguvu hii mapema ila njia wanayotumia sio sahihi ndio maana watoto wao hawajapona mpaka leo, zaidi niwashauri njooni kwa Yesu na mtaona mambo makubwa bila kutarajia.

 

 


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA

ROZARI YA KUWAOMBEA MAREHEMU TOHARANI

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

IBADA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

TAMBUA UMUHIMU WA KUOMBEA MIMBA KWA MAMA MJAMZITO

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO