SALA YA KUOMBEA JUMUIYA KWA MAOMBEZI YA MT. PADRI PIO


SALA YA KUOMBEA JUMUIYA KWA MAOMBEZI YA MT. PADRI PIO

 

Ee Mt. Pio leo tunakuja kwako tukijua kwamba kweli wewe ni mtenda miujiza, mmoja ambaye huko karibu ya Yesu. Tunakuomba utuombee kwa nia zetu mbele ya kiti cha enzi cha Mwenyezi Mungu kwa maombi yako Jumuiya yetu iwe na mshikamano \ upendo wa dhati katika kumtumikia Mwenyezi Mungu ndani na nje ya Jumuiya daima wanajumuiya tutamani kuishi maisha yampendezayo Mwenyezi Mungu katika familia zetu.

Tunasali kwa maneno ya Mt. Papa Yohana Paul II, tunakuomba sala zako kwa niaba yetu. "Adhimu, mnyenyekevu na mpendwa Padri Pio. Tunaomba utufundishe unyenyekevu wa moyo ili tuweze kuhesabiwa miongoni mwa watoto wadogo wa Injili ambao Baba aliahidi kuwafundisha siri za ufalme wake. Utusaidie tusali pasipo kukoma, tukiamini kwamba Mungu anajua tunachohitaji hata kabla ya kumwomba.

Utuombee tupate macho ya Imani yatakayotusadia kutambua katika maskini na wanaoteseka, sura halisi ya Yesu. ututunze katika saa ya mahangaiko na majaribu na kama tukianguka, basi tupate mang`amuzi ya furaha ya sakramenti ya msamaha.

Utuombee nasi tuwe na moyo kama wako wa upendo kwa Maria, mama wa Yesu na Mama yetu. Utusindikize katika hija yetu ya hapa duniani kuelekea nchi takatifu ambapo sisi pia tunamatumaini kufika ili kutafakari milele utukufu wa Baba, Mwana na roho mtakatifu. Amina".

Mt. Padri Pio kwa upendo tunasali nawe sala uliyoitunga kwa ajili ya Imani na matumaini katika huruma ya Mungu.  "Ee Bwana, tunaomba tuwe na matumaini na Imani katika huruma yako ya Kimungu na ujasiri wa kupokea misalaba na mateso ambayo yanaleta wema tele katika roho zetu na katika kanisa lako. Utusaidie tukupende wewe kwa Imani na mapendo makubwa katika Ekaristi Takatifu, na tukuruhusu wewe utende ndani yetu kama unavyotaka kwa ajili ya utukufu wako mkuu.

Ee Yesu, moyo unaoabudika sana na chemichemi ya milele ya upendo wa kimungu, tunakuomba sala yetu ikirimiwe mbele ya ukuu wa kimungu wa Baba yako wa mbinguni.

Utukufu wote uwe kwa Baba na kwa Mwana na kwa roho Mtakatifu kama mwanzo na sasa na siku zote na milele.

Mt. Padre Pio utuombee. Amina.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAHAMU JINSI YA KUOMBA SALA YA VITA

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

SALA KWA AJILI YA KUFUNGULIWA KUTOKA KATIKA NGUVU ZA GIZA

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO

IBADA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA