SALA NA FAMILIA


                                   SALA NA FAMILIA



 

Tumsifu Yesu Kristo!

Ndugu zangu wapendwa ni wazi kila mtu ametoka katika familia na kila mtu anayo familia.

Tunajua wazi tunfamilia za aina mbalimbali yaani iwe ni familia ya Baba, Mama na watoto au familia ya Mama na watoto au familia ya Baba na watoto au familia ya watoto tu wanaojilea wenyewe, zote hizo ni familia.

Mzazi Baba au Mama ni kiongozi katika familia yako, yawezekana unatimiza majukumu yote muhimu ya familia yako kwa kuhakikisha watoto wako wanapata Chakula bora, Elimu bora na Maradhi bora kabisa, yote haya ni jambo jema kabisa. Lakini katika swala la Imani au kuwasisitiza watoto kusali ukajisahau kidogo, kwa misingi hiyo, Leo nakuja kukukumbusha umuhimu wa kumjengea mtoto wako Hofu ya Mungu, Utii kwa Mungu, mahusiano mema na Mungu wake, kwa kufanya hivyo utakuwa umetimiza wajibu vema ndani ya familia yako.

Lazima ukumbuke mambo yafuatayo:-

 

1.  MALEZI YA MITANDAONI

Kumbuka hivi sasa kuna malezi mazuri na malezi mabaya yanayotolewa katika mtandao, ambayo yanaweza kukuharibia mtoto kabisa au kumjenga mtoto, na ili kushinda vita hivi vya malezi ya mtandaoni lazima mtoto wako hampende Mungu wake, awe na hofu ya Mungu.

 

2.  TABIA CHAFU KATIKA JAMII INAYOMZUNGUKA

 

Ila mtoto wako aweze kushinda tabia chafu inayomzunguka lazima awe na nguvu ya Mungu na nguvu ya Mungu anaipata katika sala. Hivyo kama familia lazima kusali.

 

3.  ULINZI WA FAMILIA

Kuna baadhi ya familia zinapata mashambulizi ya kiroho kwa sababu hazisali tu, na mashambulizi haya ni pamoja na Magonjwa yenye kulenga kudhoofisha Uchumi wa familia, watoto kukataa shule bila sababu ya msingi. Ndoa kuvunjika, watoto kuzaliwa na kupoteza maisha katika hali isiyo ya kawaida yote hayo ni kwasababu ya familia kukosa ulinzi, ni familia kumuweka Mungu mbali, ni familia kutokusali.

 

4.  KUWALINDA WATOTO WAKO NA NGUVU ZA GIZA

 

Kumbuka wazi Mungu wetu adanganyi wala adanganyiki, na wala haitaji msaada wowote toka kwa miungu unayoijua wewe, hivyo ili uweze kuilinda familia yako vyema unatakiwa kuwahimiza watoto wako kusali kwa bidii na kusoma kwa bidii, na endapo watoto wako wanaumwa wapeleke hospitali kwa matibabu na waombee au wapeleke pia kwa Yesu wa Ekaristu, tumia matibabu ya aina mbili ya hospitali na maombi ili dawa anazotumia kwa Baraka za Mungu zikatende kazi njema.

 

Kuna magonjwa mengi siku hizi ya nguvu za giza na yanafanana kabisa na magonjwa yasiyo ya nguvu za giza na bila kusali hauwezi kamwe kuyatofautisha. Na magonjwa haya yamekuwa yakiporomosha Uchumi wa familia na kufanya familia kuwa maskini kabisa, mfano wa Magonjwa hayo ni kama vile

Ø Mtoto kuugua au kupata tatizo la upungufu wa damu.

Ø Kuugua kisukari

Ø Kuugua macho

Ø Maumivu ya kichwa n.k

Magonjwa haya yapo kweli lakini mengine niyakutengenezwa katika Ulimwengu wa giza, hivyo kama familia haisali na Adui anaiwinda familia hiyo ataweza kuisambaratisha kabisa kwa urahisi kwa maana iko mbali na Mungu.

Hivyo kama wazazi lazima kuweka utaratibu wa sala ndani ya familia zetu, kukaa mbali na Mungu ni kujidanganya. Familia iliyo salama lazima itembee na Mungu sio pesa.

Familia na sala ni nguvu ya ushindi katika malezi, katika safari yetu ya hapa duniani, kwa neema ya Mungu niwatakiye wanafamilia wote kutembea na nguvu ya Mungu ndani ya familia zetu.

 

Mungu awabariki sana.

Mwl. Julius Theophil Mmbaga

Mtumishi ndani ya Familia

0766500747

TAZAMA VIDEO HII UPATE KUJIFUNZA ZAIDI



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA

MALAIKA MKUU MT. MICHAEL UTULINDE KATIKA VITA

ROZARI YA KUWAOMBEA MAREHEMU TOHARANI

SALA KWA AJILI YA KUFUNGULIWA KUTOKA KATIKA NGUVU ZA GIZA

HISTORIA YA MAISHA YA BIKIRA MARIA

FAHAMU JINSI YA KUOMBA SALA YA VITA