Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2022

SALA KUU YA YESU KRISTO

Picha
  SALA KUU YA YESU Ewe mkombozi mwenye huruma, uliyekufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu, unikinge na maovu yote yawezayo kunifikia. Ewe msulubiwa wa Nazareti, unihurumie leo na kila siku, kwa heshima ya Rabi yetu Yesu Kristu na kwa heshima ya kufufuka kwake kutakatifu, na kupaa mbinguni kwa enzi ya Umungu wake na kwa kuwa umeniumba ili nifike mbinguni. Ewe msalaba mtakatifu wa Kristu unikinge na kifo kibaya cha namna yoyote na unipe uzima kila siku. Ni hakika kuwa Yesu Kristu alizaliwa katika zizi la ng’ombe siku ya Noeli, Ewe msalaba mtakatifu wa Yesu Kristu, unikinge na maadui wangu wote. Ni hakika kuwa wafalme watatu wenye busara walileta zawadi zao kwa siku ya kumi na tatu tangu kuzaliwa kwake Kristu. Ni hakika kuwa Yesu Kristu alisulubiwa msalabani kwenye kilima cha Kalvaroo siku ya Ijumaa. Ni hakika kuwa alipaa mbinguni. Heshima ya yesu itaniondolea maadui wangu niwaonao na nisiowaona leo na siku zote. Ewe Yesu mwema unihurumie. Mama na Yosefu mlliyemwondoa Yesu msalaba

NGUVU YA SALA ALIZOFUNDISHWA MTOTO GRACE

Picha
NGUVU YA SALA ALIZOFUNDISHWA MTOTO GRACE                                             (UMRI WA MTOTO NI MIAKA 12) MNAMO MWAKA 2015 NA MALAIKA MICHAEL   UTANGULIZI Sala hizi ni sala zilizoandikwa na mtoto Grace mwenyewe, akiongozwa na Mt. Michael Malaika Mkuu, na sala hizi ziliandikwa baada ya ombi maalum toka kwangu, hii ni baada ya kutaka kudadisi Malaika wanamfundisha nini mtoto Grace awapo usingizini, maana wakati mwingine mtoto Grace akiwa kalala na ukienda kumwamsha kama nafsi yake haipo hapo, alinyoosha mkono tu kutoa ishara ya kusubiri, basi tuliweza kusubiri mpaka alipozindika peke yake.   Hata pale alipoweza kuamka ulipomuuliza alikuwa wapi, naye alijibu wakati umekuja kuniamsha, Mt. Michael Malaika Mkuu alikuwa ananifundisha sala, au anaweza kukujulisha alikuwa na Malaika Enjo au Anjelina hawa ni Malaka waliojitambulisha kwa Majina hayo ndani ya familia, basi baada ya kugundua kuna kitu kinaendelea, ndipo nilipomwomba mtoto Grace aweze kuandika sala zote anazofundish

SALA YA KUOMBEA JUMUIYA KWA MAOMBEZI YA MT. PADRI PIO

Picha
SALA YA KUOMBEA JUMUIYA KWA MAOMBEZI YA MT. PADRI PIO   Ee Mt. Pio leo tunakuja kwako tukijua kwamba kweli wewe ni mtenda miujiza, mmoja ambaye huko karibu ya Yesu. Tunakuomba utuombee kwa nia zetu mbele ya kiti cha enzi cha Mwenyezi Mungu kwa maombi yako Jumuiya yetu iwe na mshikamano \ upendo wa dhati katika kumtumikia Mwenyezi Mungu ndani na nje ya Jumuiya daima wanajumuiya tutamani kuishi maisha yampendezayo Mwenyezi Mungu katika familia zetu. Tunasali kwa maneno ya Mt. Papa Yohana Paul II, tunakuomba sala zako kwa niaba yetu. "Adhimu, mnyenyekevu na mpendwa Padri Pio. Tunaomba utufundishe unyenyekevu wa moyo ili tuweze kuhesabiwa miongoni mwa watoto wadogo wa Injili ambao Baba aliahidi kuwafundisha siri za ufalme wake. Utusaidie tusali pasipo kukoma, tukiamini kwamba Mungu anajua tunachohitaji hata kabla ya kumwomba. Utuombee tupate macho ya Imani yatakayotusadia kutambua katika maskini na wanaoteseka, sura halisi ya Yesu. ututunze katika saa ya mahangaiko na majaribu

JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA

Picha
JINSI YA KUSALI ROSARI TAKATIFU YA BIKRA MARIA   KANUNI ZA IMANI 1.    Nasadiki kwa Mungu Baba Mwenyezi muumba mbingu na dunia na kwa Yesu Kristo mwanaye wa pekee, Bwana wetu, aliyetungwa kwa uwezo wa roho mtakatifu akazaliwa na Bikra Maria akateswa kwa mamlaka ya Polystyo Pilato, akasulubiwa akafa, akazikwa akashukia kuzimu siku ya tatu akafufuka katika wafu akapaa mbinguni, amekaa kuume kwa Mungu baba Mwenyezi toka huko atakuja kwa utukufu kuwahukumu wazima na wafu, Nasadiki kwa roho Mtakatifu, Kanisa takatifu Katoliki, ushirika wa watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili na uzima wa milele ijayo Amina.   2.    BABA YETU Baba Yetu uliyembinguni jina lako litukuzwe, ufalme wako ufike utakalo lifanyike duniani kama mbingui utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyo wasamehe na sisi waliotukosea usitutiye katika kishawishi lakini utuokoe maovuni Amina.   3.    SALAMU MARIA Salamu Maria umejaa neema Bwana yu nawe umebarikiwa kuliko w