Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2023

HISTORIA YA MAISHA YA BIKIRA MARIA

Picha
  HISTORIA YA MAISHA YA BIKIRA MARIA MAISHA YA WAZAZI WA BIKIRA MARIA Mnamo karne ya pili kabla ya kuzaliwa kwake Bwana wetu Yesu kristo. Wazazi wa Bikira Maria walijulikana katika Kanisa kwa majina ya JOAKIMU na ANNA. Hata ilipofika karne ya nne, Wakristu wa kanisa la Mashariki walikuwa tayari wameshazoea kuwaheshimu wazazi hawa. Mwaka 1548 Kanisa Katoliki lilianza rasmi kusherekea sikukuu ya wazazi wa Mungu, Katika kalenda ya Kanisa sikukuu ya Watakatifu hawa huadhimishwa tarehe 26 Julai kila mwaka. BABA MZAZI WA BIKIRA MARIA Joakimu ndiye Baba mzazi wa Bikira Maria, Baba huyu alikuwa wa kabila la Yuda na Ukoo wa Mfalme Daudi. Jina Joakimu lina maana ya Matayarisho kwa ajili ya Bwana ; au Bwana anatayarisha. Mtakatifu huyu aliishi Nazareti iliyoko Galilaya. MAMA MZAZI WA BIKIRA MARIA Anna ndiye mzazi wa Bikira Maria, Mama huyu alizaliwa katika ukoo wa Haruni Kuhani Mkuu wa kabila la Yuda. Jina la Anna lina maana ya Neema au Enye Neema. Mama huyu nyumbani kwao kulikuwa Be

CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO

Picha
  CHANGAMOTO YA NDOTO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO Tumsifu Yesu Kristu, Ndugu yangu katika Makala hii napenda leo kujadili juu ya changamoto ya ndoto katika ulimwengu wa roho. Ninaposema changamoto ya ndoto katika Ulimwengu wa roho namaanisha ni hali ya mtu kuota ndoto ambazo zinafanana sana na uhalisi wake katika hali ya kawaida, yani unaota ndoto ambayo wewe mwenyewe unaona au unahisi kabisa kitu hichi ni kweli kimefanyika, mfano wa ndoto hizi ni 1)     Unaota unakula nyama mbichi na unapohamka ukitafakari hiyo ndoto na ukigusa meno yako unawez kukuta mabaki halisi ya nyama katika kinywa chako.   2)     Unaota unakula kweli na ukiamka asubuhi umeshiba kabisa wala huitaji chakula chochote.   3)     Unaota unakimbizwa, na unakimbia kweli, ukizinduka katika ndoto unajikuta ni mtu mwenye hofu na unahema kweli na kila tukio unalikumbuka vema.   4)       Unaota huko katikati ya watu waliovaa nguo nyeusi au nyekundu wanakucheka au wanakula nawe.   5)     Unaota unafanya

FAHAMU JINSI YA KUOMBA SALA YA VITA

Picha
  SALA YA VITA (0766500747) Namuungamia Mungu Mwenyezi kutokana na dhambi zangu zote nilizokutenda Bwana kwa mawazo yangu, kwa vitendo vyangu na kutotimiza wajibu wangu, Bwana unisamehe, naomba msamaha wa dhambi zangu kwa jina takatifu la Yesu Kristo Mwokozi wangu, natangaza uhuru wangu kwa damu ya Yesu Kristo wa Nazareth. Nakuja kwa Baba Mtakatifu, Mungu wangu katika jina takatifu litetemeshalo mpaka kuzimu la Bwana wetu Yesu Kristu, naomba unijalie moyo wa ujasiri, nguvu na imani katika sala hii, nipe ujasiri kama mtumishi wako Daudi katika vita na Goliati, univalishe nguvu na imani kutoka mbinguni kwa msingi wa neno lako. Sasa Mwenyezi Mungu natumia moyo wa ujasiri, nguvu na Imani uliyonijalia kupiga na kuteketeza milele mipango yote ya shetani na mawakala wake dhidi yangu, na dhidi yah ii kazi yangu na familia yangu yote katika jina la Yesu Kristo. Baba nipe mpako wa kivita kama uliompa Daudi zaburi 89:20-24 inashuhudia na ahadi yako yasema “mimi nitawaponda wapinzani wake,